UMEPONYWA NA KUEZESHWA KIMUNGU (Upako Huo Huo Uko Ndani Yako)
Scripture
KWA BIBLIA – Mathayo 16:13-16 “Basi Yesu alipofika pande za Kaisaria Filipi, aliwauliza wanafunzi wake, akisema, ‘Watu husema mimi, Mwana wa Adamu, ni nani?’ Wakasema, ‘Wengine husema Yohana Mbatizaji, wengine Eliya, na wengine Yeremia au mmoja wa manabii.’ Akawaambia, ‘Nanyi je, mnasema mimi ni nani?’ Simoni Petro akajibu, akasema, ‘Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.’”
Devotional
TUZUNGUMZE
Tyler: “Yesu alifanyaje miujiza yote hiyo?”
Mary: “Ni kwa sababu Roho Mtakatifu alimjia na kumtia mafuta. Na unajua nini? Roho Mtakatifu huyo huyo yuko ndani yako sasa.”
Neno “Kristo” linatokana na neno la Kiyunani “Christos,” ambalo linamaanisha Masihi au Aliyetiwa Mafuta, na upako wake. Kwa hivyo kinyume na kile ambacho baadhi ya watu wanaamini, “Kristo” si jina la ukoo la Yesu; badala yake, linarejelea upako unaomfanya kuwa jinsi alivyo. Upako huo ulimpa nguvu za kiungu kwa ajili ya huduma yake duniani.
Kumbuka, ingawa Yeye mwenyewe alikuwa Mungu, alihudumu kama Mwana wa Adamu alipokuwa duniani. Lakini upako uliingia katika maisha yake wakati Roho Mtakatifu alipomjia katika Mto Yordani (Yohana 1:32-33), na ndipo alipokuwa “Kristo.” Hakufanya muujiza wowote hadi upako wa Roho Mtakatifu ulipomjia na kumfanya kuwa “Kristo.” Upako huo ulimpa uwezo wa kufanya kazi kuu alizofanya.
Matendo 10:38 yasema, “…jinsi Mungu alivyomtia Yesu wa Nazareti mafuta kwa Roho Mtakatifu na kwa nguvu, naye akazunguka akitenda mema na kuponya wote waliokuwa wakidhulumiwa na ibilisi, kwa maana Mungu alikuwa pamoja naye.” Na kama Mary alivyomwambia Tyler, upako huo huo uko ndani yako ulipopokea wokovu. Roho Mtakatifu anaishi ndani yako. Hii inamaanisha wewe si wa kawaida. Umezeshwa kimungu. Kwa hivyo, unapokabiliana na mitihani, shinikizo la rika, kutokuwa na usalama, au hali ngumu, kumbuka unayo uwezo wa kiungu ndani yako. Utukufu kwa Mungu!
Confession
Baba mpendwa, asante kwa kunipa ufunuo wa Yesu kama Kristo. Pia nakushukuru kwa kunisaidia kutambua kwamba upako huo huo uliomfanya Yesu kuwa Kristo unafanya kazi ndani yangu; kwa hiyo, ninao uwezo wa kiungu wa asili wa kuleta mabadiliko na kufanya mambo makuu, kwa Jina la Yesu. Amina.
Prayer
Ee Bwana Mungu, naamini kwa moyo wangu wote katika Yesu Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai. Naamini alikufa kwa ajili yangu na Mungu alimfufua kutoka kwa wafu. Naamini yuko hai leo. Nakiri kwa kinywa changu kwamba Yesu Kristo ni Bwana wa maisha yangu kuanzia siku hii. Kupitia Yeye na kwa Jina lake, ninao uzima wa milele; mimi ni
Salvation Prayer
Ee Bwana Mungu, naamini kwa moyo wangu wote katika Yesu Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai. Naamini alikufa kwa ajili yangu na Mungu alimfufua kutoka kwa wafu. Naamini Yeye yuko hai leo.
Ninakiri kwa kinywa changu kwamba Yesu Kristo ni Bwana wa maisha yangu kuanzia siku hii. Kupitia Yeye na kwa Jina Lake, nina uzima wa milele; nimezaliwa mara ya pili.
Asante Bwana, kwa kuniokoa nafsi yangu! Sasa mimi ni mtoto wa Mungu. Haleluya!